Kiswahili Dadisi - Mazoezi ya lugha Darasa la 2, Kitabu cha Mwanafunzi


Mazoezi ya Lugha Gredi 2 Kiswahili Dadisi, Mazoezi ya Lugha ni msururu wa vitabu vipya vilivyoandikwa kwa upekee ili kutosheleza mahitaji ya mtalaa mpya wa Umilisi. Vitabu hivi vitamwezesha mwanafunzi kupata ufahamu wa lugha kupitia stadi za kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika. Aidha, vina mazoezi murua ambayo yatampa mwanafunzi hamu ya kujifunza. Pia vinakuza umilisi uliopendekezwa, maadili na kufahamisha kuhusu masualaibuka. Katika Kiswahili Dadisi, Mazoezi ya Lugha, Kitabu cha Mwanafunzi, Gredi 2, utapata: • mada zilizopangwa kwa kuzingatia muainisho wa mtalaa mpya • mifano halisi ya miktadha ambapo lugha hutumika • mazoezi nje ya darasa ili kuendeleza ujifunzaji na kuwashirikisha wanafunzi katika shughuli za kijamii zinazokuza ujifunzaji • mazoezi yanayomhusisha mwanafunzi moja kwa moja • jinsi ya kuwashirikisha wazazi na walezi ili kuimarisha uwajibikaji. Kiswahili Dadisi, Mazoezi ya Lugha, Kitabu cha Mwanafunzi kina Mwongozo wa Mwalimu ambao pia una mazoezi na maelekezo tosha ambayo mwalimu atahitaji ili kumwongoza mwanafunzi aweze kufaulu katika mtalaa huu mpya wa Umilisi.
KES 161
International delivery
Free click & collect
UPC9780195746839
Author Francis Waititu
Language Swahili
License period 1155
Format EPUB
Publisher Oxford University Press East Africa
SKU9780195746839
None

Reviews

Leave a product review
or cancel